
Kodjo Samlan wa shirikisho la soka la Afrika (CAF) amethibitisha kwamba kocha msaidizi wa togo Abalo Amnalete na afisa habari Stanislas Ocloo waliojeruhiwa ktk shambulio hilo la jana wamefariki leo saa nne kamili asubuhi.Idadi ya watu waliopoteza maisha sasa imefikia watu watatu,dereva wa basi la wachezaji alifariki jana ktk eneo la tukio.
Ripoti toka ufaransa zinasema kwamba wachezaji wa togo wameamua kutoshiriki ktk michuano hiyo itayoanza hapo kesho jumapili,togo walitarajiwa kucheza na Ghana hapo jumatatu.
No comments:
Post a Comment